Monday, February 28, 2011

LETS LOOK THE DIFFERENCES BTN US AND THEM


 NA TAZAMA HII

je tunaweza wafikia wao kwa maendeleo?inabidi tujipange tujue nini tunafanya,watanzania amkeni wote kwa pamoja tushirikiane kuutokomeza umasikini wetu huu ulio kithiri,

Tuesday, February 22, 2011

PRIVA MTANZANIA: WATANZANIA MPO

PRIVA MTANZANIA: WATANZANIA MPO



HAYA NDIO MAISHA YETU WATANZANI,
maisha yetu yamekuwa ya kutegemea mungu mda wote hatujui kesho kutakucha vipi tunasubiri miujiza ya mungu itusaidie hii ni mbaya zaidi kutembea bila kujua unakoelekea

WATANZANIA MPO

HII NDO TOFAUTI AMBAYO HUNIUMIZA NIKITIZAMA  MAENDELEO YETU NA MAENDELEO YA YAO
kila siku zinavyosogea huwa najiuliza kama nitakuja kushuhudia Tanzania ambayo itakuwa na maendeleo hama nchi zilizoendelea?huwa najiuliza maswali mengi juu ya hii nchi yangu,nawaza tufanyeje tuone maendeleo kama wenzetu?je nitakufa kabla sijaona barabara za juu na chini nchini mwangu,napata huzuni nikiona nchi za wenzetu ziko kama picha inavyoonyesha hapo juu wakati nchi yetu ikiwa  kama picha inayofuata hapo chini yake

  Ni vipi tutafanya ilii tuwe kama nchi zilizoendelea,matatizo yote haya yanaletwa na uongozi wetu mbaya,pia tamaa za madaraka unamkuta kiongozi anamadaraka zaidi ya moja,na hii hupelekea kushindwa kufanya kazi ipasavyo,niaibu kwa Taifa tangu tupate uhuru maendeleo hakuna hata kidogo.

Friday, February 18, 2011

MABOMU TANZANIA

     Nchi ya Tanzania ni miongoni mwa nchi nzuri zenye amani na upendo,tumekuwa tukiishi kwa amani mda wote huo tangu tulipo pata uhuru,
    Amani sasa imetoweka kwani kila kukicha raia wanapoteza maisha kwa uzembe wa serikari yetu,uongozi usiotazama mbele kazi yake kubwa ni kutatua matatizo ndani ya chama chao ila sio kutatua matatizo ya nchi yetu,
     Mnamo mwaka kama mmoja hivi mbagala ililipuka mabomu ktk kambi ya jeshi huko mbagala,serikali ikazungumzia tu bila kufanya utafiti juu ya mabomu mengine ktk kambi nyingine huu ni uzembe mkubwa wa serikali
      Kama serikali yetu ingekuwa inajari wanainchi wake,ingefanya utafiti juu ya kambi nyingine kuhusu kuona kama je kambi nyingine zinamabomu ambayo hayajapitwa na wakati
      Sasa Gogo la mboto,kumelipuka tena hii inaonyesha kuwa tunaongozwa na viongozi wasiojua kuangalia matukio na kuyafanyia kazi,tukio la kwanza la mbagala linge washitua serikali na kufanya utafiti yakinifu juu ya kambi zetu za jeshi,
      Huu ni uzembe ambayo sisi kama wazalendo wa nchi hii hatuwezi kuvumilia kuona nchii yetu ikipunguza wazalishaji mali wengi kwa makosa ya `uzembe wa serikali yetu.tumechoka kupoteza ndugu jamaa na marafiki zetu kwanini serikali isiweke wataalam wa kuchunguza maswala kama hayo,nchi yetu inakambi nyongi sana je tunazitizama je hizo kambi?
    Sasa tujiulize serikali yetu imejipanga vipi kukomesha milipuko hiyo ya mabomu ambayo humaliza wananchi wenzetu?katika hutuba ya rais wetu hakuzungumzia swaala la kutokomeza ulipukaji wa mabomu katika kambi zetu za jeshi,
     Itakuwaje kama baada ya mwaka mmoja sehemu itayofuata itakuwa ni lugalo?makongo? masaki?itakuwaje kwa taifa
    Serikali yapasa kutambua kuwa mambo haya ya mabomu kuna watu wanaweza kuyaweka yakawa ni mambo ya kisiasa kwani hamna mipango ya kuzuia yasitokee tena.

Thursday, February 17, 2011

WANAMUZIKI WA BONGO

Hii ni maalumu kwa wasaani wa kitanzani ,ni bora kuwa na mawazo kutoka kwa wadau wa mzik na wenye mawazo endelevu kama baadhi ya wasomi,wasomi wengi wanatakiwa wawe na mambo mengi pia wawe na mawzo kama haya
     kwanza wasaani ni watu muhimu sana katika jamii yetu,lakini kuttokana na wanavyojiweka ndo tunawashusha ktk jamii yetu.
      msaani ni kampuni ambayo ni kampuni endelevu kama akijipanga na kujiwekea malengo,kwanini nasema msanii ni kampuni?
       msanii ni kampuni kwa sababu kuu moja tu,msani yeye ndo anatakiwa aajiri watu ila sio yeye aajiriwe,kama tunavyoona wasanii wetu wakiajiriwa na promoters pamoja na ma redio presenters.
      msanii makini mwenye kutaka maendeleo anatakiwa aajiri watu ila sio yeye aajiriwe kwa msanii kuajiriwa ni kumnyonya msanii,msani bora anatakiwa anatakiwa aajiri watu wafuatao
                         msanii anatakiwa aajiri dj wake
                         msanii anatakiwa  aajiri promoter wake
                         msanii anatakiwa aajiri marketting manager wake
                         msanii anatakiwa aajiri disigner wake
                         msanii anatakiwa aajiri mshauri wake
        jamani je tanzania kuna msanii mtanzani mwenye vitu hivi,?ni kazi sana lakini mapinduzi ya muziki naamini ipo siku yatakamilika ,,,,,,,,,naamini kama msanii anaetaka kuenderea lazima ajaribu kufuata hivi.
         msanii ni kampuni kwasababu anatakiwa awalipe watu wote hao,so lazima watu hao wafanyye kazi nzuri kwa msanii ndo waweze kulipwa na msanii
 lakini hata sisi tunatakiwa tuwashauri wanamuzik wetu ili kuleta maendeleo
        wasanii wetu wamekosa vitu muhimu sana kama vifuatavyo
     ELIMU
hapa ndo tunaongelea kitu kikubwa sana  wasanii wetu hawana elimu, wanafanya kazi kwa kubahatisha tu ukiwauliza wanasema ni kpaji,au mziki upo kwenye damu au nimezaliwa nao haya ni majibu ya kitoto  sana na hayafai kusikilizwa mbele ya watu.
    MTAJI
 msanii antakiwa awe na mtaji wa kutosha ili awe bora na aweze kuwalipa watu wake ,wacheza show wake,dj wake nk.
UBUNIFU,
msanii anatakiwa awe mbunifu wa kazi zake ,wengi watanzania wasanii hujtahidi sana kuwa wabunifu lakini kuna wengine sio wabunifu matokeo yake huiga kazi za wengine na hii haipendezi kwa mwanamziki
   msanii anatakiwa awe mbunifu kuanzia kwa jina lake mwenyewe,kazi zake,picha zake,blog yake,nk
 hii ni kwa wasanii wetu wa kitanzania jamani tuwashauri wasanii wetu

Sunday, February 13, 2011

SIKU YA WAPENDANAO

Siku hii ni siku ya historia inayo husu wapenzi wa wili na mapenzi yao,kiukweli siku hii wengi huitumia kuonyeshana mapenzi yao ya dhati mf,A anamtao out B ,kimantiki out hii haina maana kwani mapenzi ya dhati kama yapo kila siku basi yaonyeshe kila siku kuwa unampenda mtu fulani ,sitafurahia kama ndani ya nyumba tunagombana then siku hii inafika nakutoa out, nakupa mazawadi mengi,alafu siku hii inapita kesho yake tunaanza kupigana tena hii haina maana
     kila siku ni siku ambayo unatakiwa kumuonyesha mpenzi wako kuwa unampenda isiwe unanidanganya leo kesho unarudia tabia yako,Siku hii wengi tunaitumia vibaya sana kwani wengi wetu siku hii tunaiweka kama ni siku ya kufanya starehe na wapenzi wetu ,wengine siku hii hupata maumivu kwani huachika na wapenzi wao,wengine hufumania wapenzi wao,
   Cha umuhimu kuja hii ilikuwa ni siku ya huzuni ktk historia ya wapenzi wale wawili duniani kwani huwezi ukasherekea harusi wakati kuna msiba nyumbani kwako tusiwe wajinga WATANZANIA WENZANGU.
     Mapenzi ya dhati yapo tu,hakuna siku maalum  ya kumuonyesha mpenzi wako kuwa unampenda sana kuliko siku nyingine siku hiyo ikipita na mapenzi yanakwisha kabisa.
   Wapenzi hebu fikirieni hilo tunasahau kuwa tunaowakumbuka watu waliokufa siku kama ya leo,vipi tunafanya vitu vingine vya ajabu hii ni siku ya huzuni duniani na si kama tunavyoifurahia baadhi yetu

Saturday, February 12, 2011

KWA WASIO MJUA PRIVA, ni mjukuu wa mkulima

Wengi huongea vitu tofauti kuhusiana na kijana huyo, sasa ebu mjueni vizuri mkiwa mnamzungumzia mjue mnaloongea juu yake,

Tuesday, February 8, 2011

KWANINI WASOMI WENGI HUENDA NJE KUFANYA KAZI

Hii ni kwa watanzania mlio nje ya nchi yetu,tulio baki Tanzania tunajua sababu nyingi zinazowafanya muende nje kufanya kazi na kuziacha nchi zenu ktk hali ya kukosa watalam  na wasomi kama nyie
 SABABU
 Zipo sababu nyingi sana  mfano, umasikini wa nchi zenu,nhi kama Tanzania inawataalamu wengi ambao wapo njee sababu za wataalam hao kwenda huko ni umasikini uliokithiri wa kitanzani,tujitahidi kuuondoa huu umaskini uliokithiri japo kwa asilimia 40 tu
    Serikali mbovu,serikali yetu ni mbovu kiasi kwamba inakuwa haina mikakati madhubuti juu ya swala zima la kuwalipa wageni mishahara mikubwa kuliko wafanyakazi wa ndani hii inawafanya wazawa kujiona hawathaminiwi ndani ya nchi yao ndo huamua kwenda nje kutafuta kazi.
     Uchanga wa taifa letu,ndugu zangu wa nje taifa linajitahid kuwapeleka nje kusoma ,lakini mnachukulia uchanga wa taifa letu kama sababu ya kuwafanya msirudi kwenu kufanya kazi,muwe mnarudi kwenu kuinua uchumi wa nchi zenu
                                          umasikini wa nchi yetu ndo hupelekea wasomi kwenda nje

                                             moja ya jengo la chuo cha udom
      
     

PRIVA KTK POZI

mda mwingine inatakiwa uwe unapumzisha kichwa ili mtu upate kuwa fresh katika kuwaza
          Nikijana mpole,mcheshi utanashati napia ni mpenda watu mpenda maendeleo,
          Mnakaribishwa kutoa mawazo

Saturday, February 5, 2011

UMASIKINI NCHINI TANZANIA

Imesemekana kuwa UMASIKINI wa watanzania haujaanza leo,upo tangu enzi za mababu zetu ,hii ni kutokana na kuwa wazee wetu hawakuwekeza katika ELIMU hivyo watanzania walio wengi hushindwa kujikimu kimaisha kwa sababu hawana ELIMU ya kutosha.
      Baadhi ya wasomi wa dunian wamejadili juu ya UMASIKINI  na kudai upo umasikini wa
                    (a)KIPATO
                    (b)ELIMU
   je WATANZANIA  tumeandamwa na UMASIKINI wa aina gani?